Friday, 10 October 2014

PEUPEEEE TRAFFIC BARABARANI WAKUTWA KTK HARI YA FEDHEHA.TAMKO LATOLEWA

TASKARI


Ama hakika sasa dunia sasa ni kijiji, na inatubidi sana kuangalia matendo yetu na picha unazozipost katika mitandao ya kijamii, maana inasambaa kama moto unaoteketeza pori. juzi nilikuwa nikipokea na kuona picha ya askari wawili wa usalama barabarani wakiwa katika hali ya kimapenzi, picha ikiwaonyesha wakiwa wana-kiss huku wakiwa kazini na sare za kazi.
Imeaminika kuwa wawili hao ni Trafick kutoka mkoa wa Kagera, na kwa taarifa zilizopo sasa ni kuwa tayari Jeshi la Polisi Kagera limechukua uamuzi wa  kuwafukuza kazi askari hawa wawili pamoja na askari aliepiga picha hii kupitia simu yake ya mkononi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Henry Mwaibambe amewataja askari hao kuwa ni PC Asuma Mpaji Mwasumbi mwenye namba F.7788, PC Fadhili Linga mwenye namba G 2122 na PC Veronica Nazaremo Mdeme na wote walikuwa askari wa kikosi cha usalama barabarani wilayani Missenyi.
Kamanda Mwaibambe amezungumza na ITV na kusema askari hao walitenda kosa hilo la fedhea kwa kupiga picha kinyume na maadili ya jeshi hilo mwaka 2012 wakiwa kazini na kwamba PC Fadhili ndiye aliyehusika na kupiga picha hizo kwa kutumia simu yake ya mkononi na kuituma katika mitandao mbalimbali ya kijamii kitendo ambacho ni kinyume cha maadili kwa sababu mbalimbali.
Mwaibambe amekiri kuwa picha husika inayoonekana kwenye mitandao ni picha halisi ambayo haijachakachuliwa hivyo ni wazi kila askari kujua maadili ya kijeshi yapo kisheria na askari yeyote anafundishwa namna ya kuishi katika maisha ya utumishi wa jeshi la Polisi.
 
chanzo: DJ FETY BLOG

Related Posts:

  • PATA KUJUA FAIDA YA DAFU. v\:* {behavior:url(#default#VML);} o\:* {behavior:url(#default#VML);} w\:* {behavior:url(#default#VML);} .shape {behavior:url(#default#VML);} Normal 0 false false false false EN-GB … Read More
  • RESASONS TO DRESS SHARP 5 Reasons Why Young Men Should Dress Sharp It only makes sense then that they should start dressing as such. It may seem superficial, but the harsh reality is that a young man is judged by others within seconds of … Read More
  • VIFO VYAZIDI TANZANIA-AJARI YAKUTISHA HABARI KAMILI KONTENA LALALIA BASI LAUA 42 LAJERUHI 23 Basi la Majinja likiwa limeangukiwa na kontena na kusababisha vifo katika eneo la Changalawe mafinga. Picha na Francis Godwin Muf… Read More
  • CHENGE KUIBUA MPYA-MAHAKAMA KUU YAKILI CHENGE AKATA RUFAA ASIHOJIWE Baraza la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kwa mara nyingine leo limeshindwa kumuhoji Mbunge wa Bariadi Magharibi kupitia CCM Andrew Chenge. Baraza hilo limeshindwa kumuhoji … Read More
  • REAKING NEWZ KUTOKA IRINGA- PANUKA MJI MZIMA Ni baada ya Polisi Kuuwa Raia Leo mapema polisi walivamia eneo la kilabuni na kuanza kupiga kila raia na kusababisa kifo cha huyo mama muuza Pombe za kienyeji. Kosa ni kufungua kilabu cha Pombe kabla ya muda u… Read More

0 comments:

Post a Comment